Test Your Bible Knowledge.

12345678910111213141516171819202122
Across
  1. 3. Ni kipimo gani katika nyakati za kale kilicholingana na homeri na bathi kumi? (Luka 16:7)
  2. 4. Mshahara wa dhambi ni nini? (Waroma 6:23)
  3. 6. Ni Mwisraeli gani mashuhuri aliyekuwa na wana “wasiofaa kitu”? (1 Samweli 2:12)
  4. 7. Ni nani aliyeitwa “mama ya kila mtu anayeishi”? (Mwanzo 3:20)
  5. 9. Yesu alimpa Simoni mwana wa Yohana jina gani? (Yohana 1:42)
  6. 10. Wanafunzi wa Yesu walikuwa wakivuta makasia kuelekea jiji gani walipomwona Yesu akitembea juu ya bahari? (Marko 6:45-49)
  7. 12. Nyuzi ndefu katika chombo cha kufumia huitwaje? (Isaya 38:12)
  8. 14. Mtu yeyote anayetaka kuwa wa kwanza kati ya ndugu zake anapaswa kuwa nani wao? (Marko 10:44)
  9. 16. Ni mwana yupi wa Noa aliyefanya jambo lililosababisha mwana wake, Kanaani, alaaniwe? (Mwanzo 9:22-25)
  10. 18. Yehova alimwagiza Abramu aondoke jiji gani la Wakaldayo? (Mwanzo 11:31; 12:1)
  11. 19. Ni eneo la kabila gani ambalo baadaye liliwakilisha eneo la kaskazini kabisa mwa nchi ya Israeli? (Waamuzi 20:1)
  12. 21. Ni ofisa gani Mroma wa Yudea aliyemwacha Paulo akiwa amefungwa kwa sababu ya kutaka kupata kibali cha Wayahudi? (Matendo 24:27)
  13. 22. Daudi alikubali kupewa adhabu gani kati ya zile adhabu tatu alizowekewa kwa kukosa kumtii Mungu na kuwahesabu Waisraeli? (2 Samweli 24:12-15)
Down
  1. 1. Ili kuonyesha ukuu wa Yehova, Isaya alisema kwamba Yehova anaweza kupima “maji” katika nini Wake? (Isaya 40:12)
  2. 2. Makao ya Adamu na Hawa yaliitwaje? (Mwanzo 2:15)
  3. 4. Gavana Feliksi alihakikisha kwamba Paulo ametoka katika jimbo gani? (Matendo 23:34)
  4. 5. Mama ya Sulemani alimfumia nini siku yake ya arusi? (Wimbo wa Sulemani 3:11)130 Y
  5. 8. Ni vazi gani lililofanana na aproni ambalo kuhani mkuu alivaa juu ya koti lake la buluu lisilo na mikono? (Kutoka 28:4, 31)
  6. 11. Ni nani aliyekuwa mkuu wa jeshi la Absalomu, wakati Absalomu alipoasi dhidi ya Daudi, kisha akawa mkuu wa jeshi la Daudi baada ya Absalomu kuuawa? (2 Samweli 17:25; 19:13)
  7. 13. Malaika aliyemweleza Maria kwamba alikuwa amechaguliwa kumzaa Yesu, aliitwa nani? (Luka 1:26-31)
  8. 15. Katika siku za Sulemani, ni kundi gani la meli lililobeba fedha, pembe za tembo, sokwe, na tausi hadi Israeli? Meli za______(1 Wafalme 10:22)
  9. 17. Ni jiji gani lililokuwa la pili kutekwa na Waisraeli walipovamia Kanaani? (Yoshua 8:18, 19)
  10. 20. Yule mtu aliyepooza ambaye aliponywa na Petro aliyekuwa amelala juu ya kitanda chake kwa miaka minane aliitwaje? (Matendo 9:33, 34)